MBUNGE WA ARUMERU MASHARIKI MHESHIMIWA NASSARI
Monday, April 2, 2012
Thursday, March 22, 2012
Saturday, October 22, 2011
AJALI YA NDEGE MKOANI ARUSHA
RUBANI wa ndege ndogo aina ya Piper Pa 34- 300 namba 5H-QTE, mali ya World Quality
Travel and Tour Limited, Ally Harun (24), mkazi wa Arusha, amekufa huku rubani msaidizi
Lilian Koima, akijeruhiwa na kukimbizwa katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC Kilimanjaro, baada ya ndege hiyo kuanguka Arumeru.
Akizungumza na waandishi wa habari, Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Akili Mpwapwa, alisema ndege hiyo ilikuwa na marubani wawili ambao ni marehemu na mwenzake Lilian Koima, ambaye hajajulikana umri wake na makazi yake, wakitokea Dar es
Salaam na kuelekea uwanja wa ndege wa Arusha.
Alisema ndege hiyo ikiwa angani saa 1.46 usiku na ikiwa imekaribia uwanja wa Arusha kutua, ilishindwa kutua kwa sababu ya giza nene kutanda uwanjani hapo na kulazimika kubaki angani.
“Wakati wakiwa angani mmoja wa rubani hawa akapiga simu Tower Control wa Uwanja wa (KIA) na kuomba kutua huko, nao aliwaruhusu na wakiwa njiani kuelekea huko, ilianguka katika kijiji cha Samaria kata ya Kikatiti, Arumeru na mawasiliano yakakatika ghafla kati yao na KIA,” alisema Mpwapwa.
Alisema ndege hiyo ilianguka karibu na nyumba ya Maria Akyoo na kuharibika na kuua mbuzi watatu walioangukiwa papo hapo, pia kibanda cha biashara kiliharibiwa.
Kamanda Mpwapwa alisema Ally alikufa papo hapo huku Lilian akijeruhiwa na kukimbizwa KCMC. Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya Mkoa ya Mount Meru.
Alisema chanzo cha ajali hiyo bado hakijajulikana na Polisi inaendelea na uchunguzi. Meneja wa Uwanja wa Ndege wa Arusha, Simon Kimiti, alisema kwa njia ya simu kuwa hatakiwi kujibu lolote na anayetakiwa kuzungumzia suala hilo ni watu wa uwanja wa ndege wa kimataifa wa
Kilimanjaro - KIA.
Taarifa ya Wizara ya Uchukuzi iliyotolewa jana ilisema ndege hiyo yenye injini mbili na uwezo wa kubeba abiria sita ni mali ya Mawala Advocates na ilikuwa ikisafiri kutoka Uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam kwenda Kilimanjaro.
Kwa mujibu wa Edward Mkiaru aliyesaini barua hiyo kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya
Uchukuzi, wakaguzi wa ajali za ndege kutoka Wizara hiyo wako Kilimanjaro kuchunguza chanzo cha ajali.
Wednesday, August 10, 2011
KONDOO MWENYE KORANI AZALIWA
KIJIJI cha Uduru wilayani Hai mkoani Kilimanjaro kimegeuka eneo la utalii baada ya waumini wa madhehebu ya Kiislamu kutoka maeneo mbalimbali wilayani humo na maeneo jirani, kwenda kumshuhudia kondoo aliyezaliwa ameandikwa maneno mwilini kwa lugha ya Kiarabu.
Waumini hao walifurika kijijini hapo juzi baada ya sala ya Ijumaa kumshuhudia kondoo huyo aliyezaliwa wiki tatu zilizopita na kuacha watu midomo wazi kutokana na kuwa na maandishi yanayosomeka kiarabu ubavuni, yakitafsiriwa kwa Kiswahili kama Yasini.
Kondoo huyo aliyezaliwa katika familia moja ya waumini wa dini ya Kikristo, aliwavuta
waumini wengi kijijini hapo na kutoka nje ya wilaya na mkoa wa Kilimanjaro kwa ajili ya kushuhudia tukio hilo la ajabu na la kihistoria ambalo halijawahi kutokea.
Grace Massawe (55) alisema kondoo huyo alizaliwa takribani wiki tatu zilizopita na hakuwahi kutambua kwamba beberu huyo alikuwa na maandishi hayo, kutokana na kutotolewa nje na mama yake.
Grace alisema baada ya kondoo huyo kuzaliwa, mama yake alibadilisha tabia na kukaa ndani ambapo awali alikuwa akila chakula nje na wenzake, lakini aligundua maandishi hayo baada ya kumtoa nje mwenyewe.
Alisema awali aliona herufi ya W yenye rangi ya dhahabu, lakini siku zilivyozidi kwenda neno hilo lilizidi kukua na kubadilika rangi na kuwa jeupe zaidi, hali iliyompa wasiwasi na kutafuta msaada ili kutambua maana ya maandishi hayo kutoka kwa waumini wa Kiislamu.
“Baada ya waumini wa Kiislamu kufika hapa nyumbani walibaini maandishi hayo ubavuni mwa kondoo huyo kuwa ya Kiarabu yanayosomeka kuwa Yasini,” alisema Grace.
Alisema waumini hao walimweleza kuwa neno hilo ni muhimu sana katika Kitabu Kitakatifu cha Korani, ambalo ni kama kitovu cha kitabu hicho, pia ni moja ya sura muhimu ndani ya kitabu hicho.
Katika hatua nyingine, Grace alisema katika ufugaji wake wa kondoo hakujawahi kutokea tukio la ajabu kama hilo na kueleza kuwa kondoo aliyemzaa alikuwa ni uzao wake wa mara ya pili ambapo awali alizaa kondoo wa kawaida.
Alisema kutokana na kondoo huyo kuvuta hisia za watu wengi, pia viongozi wakubwa wa dini hiyo walifika kushuhudia maajabu hayo, akiwamo Katibu wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) wa Mkoa wa Kilimanjaro, Shehe Rashid Mallya, na Shehe Mkuu wa Wilaya ya Hai, Juma Lyimo.
Juhudi za kumtafuta Shehe Mallya kuzungumzia tukio hilo, zilishindikana baada ya simu yake kuita bila kupokewa.
Waumini hao walifurika kijijini hapo juzi baada ya sala ya Ijumaa kumshuhudia kondoo huyo aliyezaliwa wiki tatu zilizopita na kuacha watu midomo wazi kutokana na kuwa na maandishi yanayosomeka kiarabu ubavuni, yakitafsiriwa kwa Kiswahili kama Yasini.
Kondoo huyo aliyezaliwa katika familia moja ya waumini wa dini ya Kikristo, aliwavuta
waumini wengi kijijini hapo na kutoka nje ya wilaya na mkoa wa Kilimanjaro kwa ajili ya kushuhudia tukio hilo la ajabu na la kihistoria ambalo halijawahi kutokea.
Grace Massawe (55) alisema kondoo huyo alizaliwa takribani wiki tatu zilizopita na hakuwahi kutambua kwamba beberu huyo alikuwa na maandishi hayo, kutokana na kutotolewa nje na mama yake.
Grace alisema baada ya kondoo huyo kuzaliwa, mama yake alibadilisha tabia na kukaa ndani ambapo awali alikuwa akila chakula nje na wenzake, lakini aligundua maandishi hayo baada ya kumtoa nje mwenyewe.
Alisema awali aliona herufi ya W yenye rangi ya dhahabu, lakini siku zilivyozidi kwenda neno hilo lilizidi kukua na kubadilika rangi na kuwa jeupe zaidi, hali iliyompa wasiwasi na kutafuta msaada ili kutambua maana ya maandishi hayo kutoka kwa waumini wa Kiislamu.
“Baada ya waumini wa Kiislamu kufika hapa nyumbani walibaini maandishi hayo ubavuni mwa kondoo huyo kuwa ya Kiarabu yanayosomeka kuwa Yasini,” alisema Grace.
Alisema waumini hao walimweleza kuwa neno hilo ni muhimu sana katika Kitabu Kitakatifu cha Korani, ambalo ni kama kitovu cha kitabu hicho, pia ni moja ya sura muhimu ndani ya kitabu hicho.
Katika hatua nyingine, Grace alisema katika ufugaji wake wa kondoo hakujawahi kutokea tukio la ajabu kama hilo na kueleza kuwa kondoo aliyemzaa alikuwa ni uzao wake wa mara ya pili ambapo awali alizaa kondoo wa kawaida.
Alisema kutokana na kondoo huyo kuvuta hisia za watu wengi, pia viongozi wakubwa wa dini hiyo walifika kushuhudia maajabu hayo, akiwamo Katibu wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) wa Mkoa wa Kilimanjaro, Shehe Rashid Mallya, na Shehe Mkuu wa Wilaya ya Hai, Juma Lyimo.
Juhudi za kumtafuta Shehe Mallya kuzungumzia tukio hilo, zilishindikana baada ya simu yake kuita bila kupokewa.
Saturday, June 11, 2011
Monday, May 16, 2011
PICHA SIKU YA KIMATAIFA YA FAMILIA
UMOJA WA VIJANA WA CHAMA CHA MAPINDUZI [UVCCM] UMESHIRIKI KATIKA KUFANYA USAFI NA KUWaFARIJI WAGONJWA KATIKA HOSPITALI KUU YA SERIKALI YA MKOA WA ARUSHA YA MOUNT MERU IKIWA NI SEHEMU YA MAADHIMISHO YA SIKU YA KIMATAIFA YA FAMILIA,KUSHOTO MJUMBE WA BARAZA KUU LA TAIFA LA UMOJA HUO NA MBUNGE WA VITI MAALUMU CATHERIN MAGIGE AKIWA NA MMOJA YA WATOTO WALIOZALIWA KATIKA HOSPITALI HIYO NA KULIA NI MAKAMU MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA ARUSHA ANNA MSUYA
Wednesday, May 11, 2011
Subscribe to:
Posts (Atom)